shahidi
Sheria

Masharti ya Matumizi

Imesasishwa: Mei 2026

1. Kukubali Masharti

Kwa kufungua account, kupakua app, au kutumia tovuti ya Shahidi, unakubali masharti haya. Kama hukubali, usitumie huduma.

2. Shahidi ni nini (na sio nini)

Shahidi ni:

  • Mfumo wa kurekodi ushahidi (audit ledger) wa mizigo ya mtandaoni
  • Channeli ya kuwapelekea pande SMS na push notifications
  • Mfumo wa kuhesabu sifa ya umma ya muuzaji na msafirishaji

Shahidi si:

  • App ya malipo. Hatupokei pesa zako; mteja na muuzaji wanawasiliana wenyewe
  • Kampuni ya bima. Hatufidi mizigo iliyoharibika au kupotea
  • Mfumo wa courier. Hatubebi mizigo; basi makampuni mengine yanafanya hivyo
  • Mfumo wa kusuluhisha migogoro. Hatuamui nani ana haki
  • Mfumo wa KYC. Tunatumia nambari ya simu kama identity, hatuhakiki ID za serikali

3. Account yako

Una account moja kwa nambari moja ya simu. Account inafungwa kwa kifaa kimoja kwa wakati mmoja (single-device kwa MVP). Wewe pekee unawajibika kuhusu shughuli zinazotokea kwenye account yako.

Lazima:

  • Uwe na umri wa miaka 18 au zaidi
  • Utoe nambari halali ya simu unayoidhibiti
  • Usiruhusu mtu mwingine kutumia account yako

4. Matumizi yanayokubalika

HUTAKIWI:

  • Kutengeneza mizigo bandia kwa ajili ya kuongeza sifa yako
  • Kuingia hila ili kuongeza idadi ya "zilizopokelewa salama" bila kweli kutuma mizigo
  • Kushirikiana na pande nyingine ku-bypass mfumo wa pin za SMS
  • Kuwasumbua wengine kupitia SMS au push (mfumo unaweka rate limits, lakini ujibu pia ni wajibu wako)
  • Kutumia mfumo kwa shughuli haramu (silaha, madawa ya kulevya, n.k.)
  • Ku-scrape au kupata data ya wengine bila idhini (per-parcel lookup ni ya hadharani, lakini scraping ya hifadhidata yote inakatazwa)
  • Ku-attack mfumo kwa njia za kiufundi (DoS, brute force, n.k.)

Tukigundua matumizi yasiyokubalika, tunaweza kusimamisha account yako mara moja. Sifa ya zamani inabaki (ndio nia ya mfumo wa monotonic).

5. Ripoti za udanganyifu

Kama mteja, una haki ya kuripoti mzigo wowote uliokupokea ukiwa umeharibika au una udanganyifu. Ripoti zako:

  • Hazibadiliki baada ya kutumwa (immutable) — hata wewe mwenyewe huwezi kuhariri
  • Zinaonekana kwenye hati ya ushahidi ya mzigo huo
  • Zinabaki kama ushahidi kwa migogoro ya nje ya mfumo (Shahidi haisuluhishi mgogoro yenyewe)

Kwa kuwajibika, usitume ripoti za uongo. Ripoti zako zinaweza kuwa ushahidi dhidi yako kama zinaonyesha mwelekeo wa udanganyifu.

6. Mfumo wa sifa (reputation)

Sifa ni nguzo ya mfumo. Sheria zake:

  • Inakua tu — idadi haipungui kamwe, hata baada ya muda mrefu
  • Idadi mbili kwa muuzaji — zilizopokelewa salama na zilizoharibika. Wateja wanaona zote mbili
  • Ni ya hadharani — mtu yeyote anaweza kuona kwa kutumia nambari ya mzigo wako au phone number yako
  • Imefungwa kwa nambari yako ya simu — ukiibadilisha simu, sifa inabaki na akaunti hiyo

Hatuwezi kufuta au kupunguza sifa yako, hata kama unaomba. Hii ni feature, sio bug — kama tukianza kufuta sifa, mfumo wote unapoteza maana yake.

7. Hati za ushahidi (evidence documents)

Muuzaji au mteja anaweza kuzalisha kiungo cha hati ya ushahidi cha mzigo wowote walioshirikiana naye. Kiungo:

  • Kinaisha baada ya siku 30 (kiotomatiki)
  • Kinaweza kubatilishwa na mtoa kiungo wakati wowote
  • Kinaonyesha taarifa za mzigo zilezile zinazoonekana kwenye app ya pande hizo — hakuna taarifa za ziada zinazofunuliwa

Kwa kuwajibika, shiriki kiungo tu na pande zinazohitaji kuona (mwenzi wa biashara, mediator, n.k.). Mara ukishiriki, mtu mwingine anaweza kushiriki tena.

8. Wajibu na vikomo

Shahidi hairesponsi kwa:

  • Pesa ulizolipa kwa muuzaji ambazo hujapata bidhaa
  • Bidhaa zilizopotea au kuharibika njiani
  • Migogoro kati ya muuzaji na mteja
  • Hasara za kibiashara zinazotokana na kuchelewa kwa mzigo

Wajibu wetu mkuu ni kurekodi vile vinavyotokea kwa usahihi. Tukifanya kosa la kiufundi (mfano, kupoteza data yako), tutarekebisha kwa kadiri tunavyoweza.

Hatutoi dhamana yoyote (warranty) — huduma inatolewa "kama ilivyo." Tunafanya kazi kuhakikisha mfumo ni wa kuaminika lakini hatuhakikishi 100% uptime au usahihi.

9. Ada na malipo

Bei zetu zimo kwenye ukurasa wa bei. Kufikia sasa (pilot):

  • Mizigo 3 ya kwanza ni bure milele
  • Baada ya hapo, ziada ya TZS 500 kwa mzigo, au tier ya kila mwezi
  • Hatuna refund kwa mizigo iliyoshakamilika
  • Malipo yanafanyika kupitia mobile money — tumia mtandao wowote unaopendelea

10. Kusimamisha au kufunga huduma

Tunaweza kusimamisha au kufunga account yako tukiona unakiuka masharti haya. Wewe unaweza kufuta account yako wakati wowote (kupitia app au kwa kuwasiliana nasi).

Tukifunga shughuli zetu zote (mfano, kampuni kufungwa), tutawajulisha angalau siku 30 mapema na kutoa nafasi ya ku-export data yako.

11. Sheria zinazotumika

Masharti haya yanaongozwa na sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kama kuna mgogoro kati yetu, tutajaribu kuusuluhisha kwa mazungumzo kwanza. Ukishindikana, mahakama za Tanzania zitakuwa na mamlaka.

12. Mabadiliko ya masharti

Tunaweza kusasisha masharti haya. Mabadiliko makubwa tutawajulisha kupitia app + email. Kuendelea kutumia mfumo baada ya mabadiliko kunachukuliwa kama kukubali.